TFF YATAJA VIINGILIO MECHI YA SIMBA NA YANGA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara(VPL) msimu wa 2017/2018 kati ya Simba na Yanga utakaochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Katika mchezo huo namba utakaofanyika saa 10 jioni Kiingilio cha chini kitakuwa shilingi Elfu Saba(7,000) wakati kiingilio cha juu kitakuwa shilingi Elfu Thelathini.
Jukwaa la VIP A itakuwa shilingi Elfu Thelathini (30,000),VIP B na C shilingi Elfu Ishirini (20,000) na Upande wa Mzunguko kwenye viti vya rangi ya Chungwa,Bluu na Kijani itakuwa shilingi Elfu Saba (7,000)
Viingilio vimetangazwa mapema wiki mbili kabla ili kuwapa nafasi mashabiki wengi kununua tiketi ili kuepuka usumbufu siku zikibaki chache.
Tiketi tayari zimeanza kupatikana kuanzia sasa kupitia Selcom

No comments

Powered by Blogger.