RUFAA YA WAMBURA YAGONGA MWAMBA TFF


Kamati ya Maadili ya Rufaa ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) imetupilia mbali Rufaa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la mpira wa Miguu Ndugu Michael Richard Wambura ya kufungiwa maisha kujihusisha na soka.

Akisoma hukumu rufani hiyo Mwenyekiti wa kamati ya Rufaa ya Maadili ya TFF, Wakili Ebenezer Mshana amesema Mawakili wa mrufani walishindwa kujibu hoja za mteja wao, kufanya hivyo na kamati yake imeridhia hukumu iliyotolewa na Kamati ya Maadili na kumtaka Wambura kuendelea na adhabu ya kufungiwa maisha kujihusisha na soka.

Wambura alihumiwa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho hilo mapema mwezi machi  kutojihusisha na soka maisha kwa makosa matatu.

(i)                 kupokea pesa za malipo yasio halali kinyume na sheria
(ii)               Kughushi barua ya kampuni ya JEKC ili kulipwa isivyo halali
(iii)             Kufanya vitendo vilivyovunja hadhi ya TFF.

"Hoja zote tatu alizotuhumiwa hakuna sehemu yoyote kwenye ushaidi wao ambayo walikanusha kutenda kosa hilo, hivyo kamati imeridhia bila shaka na hukumu iliyotolewa awali na Kamati ya nidhamu," alisem Mshana.

No comments

Powered by Blogger.