KLOOP AWAONYA NYOTA WAKE MECHI YA MARUDIANO YA ROMA


Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amewaonya wachezaji wake kutobweteka na ushindi wa mabao 5-2 iliyopata jana dhidi ya AS Roma katika nusu fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya kwakua miamba hiyo ya Italia inaweza kupindua matokeo kwenye mechi ya marudiano.

Mjerumani huyo amewasisitiza wachezaji wake kuwa mchezo huo bado haujamalizika wanatakiwa kuhakikisha wanashinda kwenye mechi ya marudiano.

Kloop amesema amejifunza kitu kikubwa katika mchezo huo kuwa wanaweza kushinda jijini Roma ingawa wapinzani wao wataingia kwa kasi ya kutafuta mabao.
"Sisi sio Barcelona wenzetu wako bora ni miongoni mwa timu tatu bora duniani, wameshinda mataji mengi lakini tutaenda Roma kutafuta ushindi kwa hali yoyote ingawa itakuwa mechi ngumu kwa upande wetu," alisema Klopp.

Katika mchezo wa kwanza wa robo fainali Roma ilikubali kipigo cha mabao 4-1 kabla ya kuibuka na ushindi wa 3-0 kwenye mechi ya marudiano kitu ambacho Klopp hataki kitokee.

No comments

Powered by Blogger.