YANGA YATUPWA NJE NA TOWNSHIP YAANGUKIA SHIRIKISHO

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika Yanga, wameondolewa katika michuano hiyo leo baada ya sare ya 0-0 waliyoipata katika mchezo wao wa marudiano dhidi ya Township Rollers ya Botwana katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Gaborone huko Botswana.

Yanga wametolewa kwa jumla ya mabao 2-1 ambayo yote yalipatikana katika mchezo wa kwanza uliopigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

Mchezo haukua mwepesi kwa Yanga ingawa walifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti washambuliaji hatari wa Rollers ambao walikua wakiishambulia Yanga kwa muda mrefu lakini walinzi wakiongozwa na Kelvin Yondani waliweza kuwadhibiti huku golikipa Youthe Rostand akilazimika kuokoa mipira kadhaa ya hatari

Yanga wao pamoja na kujitahidi sana lakini walifanikiwakutengeneza nafasi moja pekee ya wazi katika dakika ya 70 baada ya Pappy Tshishimbi kuupenyeza mpira uliomkuta Obrey Chirwa katika nafasi nzuri lakini hata hivyo shuti la Chirwa halikulenga lango.

Kwa matokeo hayo sasa, Yanga wataangukia katika hatua ya mtoano ya kombe la shirikisho.

No comments

Powered by Blogger.