UKAME WA MABAO WAMUUMIZA KICHWA GIROUD
Mshambuliaji wa Chelsea, Olivier Giroud amekiri kuwa
anaumia kushindwa kufunga mabao akiwa na matajiri hao wa London.
Mfaransa huyo amefunga bao moja tangu ajiunge na
timu hiyo akitokea Arsenal mwezi Januari huku akisaidia mabao matatu katika
mechi nane alizocheza mpaka sasa.
Giroud 30, hana uhakika wa kuwemo kwenye kikosi cha
Ufaransa kitaka choshiriki kombe la dunia na moja ya sababu iliyomfanya kuondoka
Arsenal ili kupata nafasi.
Ingawa ameanza kwa changamoto maisha yake ndani ya
Chelsea, Giroud anaamini atafanikiwa zaidi akiwa Stamford Bridge.
“Nina furaha kwa jinsi nilivyoweza kuzoea mazingira
ya hapa, pia jinsi nilivyopokelewa na ushirikiano ndani ya uwanja ninaopata
kutoka kwa wachezaji wenzangu.
"Natakiwa kufunga mabao mengi zaidi, kwa mujibu
wa takwimu nimefunga bao moja na kusaidia mengine matatu tangu nije hapa,"
alisema Giroud.
No comments