SAMUEL UMTITI NJIA NYEUPE KWENDA MAN UNITED


Habari zilizoripotiwa na mtandao wa SPORT nchini Spain zinaeleza kwamba Barcelona wanajiandaa kuachana na beki wake raia wa Ufaransa Samuel Umtiti. 

Umtiti amehusishwa Kwa kiasi kikubwa kuhamia Manchester United msimu ujao kufuatia makubaliano kuongezwa mshahara ili asaini mkataba mpya na Barcelona kuyumba kwani mchezaji huyo anataka alipwe kiasi cha pesa anacholipwa Andreas Iniesta kitu ambacho Barcelona hawakubaliani nacho. 

Paundi milioni 50 ndizo hasa zinazoweza kumtoa mchezaji huyo Barcelona kabla ya mkataba wake kumalizika na tayari United wameonyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo wakiwa tayari kulipa kiasi cha mshahara  anachotaka. 

Umtiti amebakiza miaka mitatu kuitumikia Barcelona na klabu hiyo ilimpa tu kipaumbele cha kujadiliana nae kuhusu mkataba mpya. 

Wakati huu ambao Barcelona wanajiandaa kumsajili Antoine Griezman ambaye atalipwa si chini ya Paundi milioni 13 Kwa mwaka, wanapaswa kupunguza matumizi yao pia na hii inaleta ugumu Kwa Umtiti kubaki. 

Tayari Clement Lenglet kutoka Sevilla ambaye anapatikana Kwa kiasi cha Paundi milioni 26 tu anatajwa huenda akasajiliwa kuchukua nafasi ya Umtiti Barcelona.



No comments

Powered by Blogger.