MAKAMU WA RAIS TFF AFUNGIWA MAISHA KWENYE SOKA.

Jina la Michael Wambura limeingia tena katika vichwa vya habari za soka la Bongo baada ya leo kukumbana na adhabu ya kufungiwa maisha kujihusisha na maswala yote ya Soka baada ya kukutwa na hatia katika makosa matatu ya kimaadili.

Michael Wambura ambaye ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) amekutwa na makosa matatu ya kimaadili ambayo yalifanyika miaka 14 iliyopita.

Akisoma hukumu hiyo Afisa habari wa shirikisho la Soka nchini TFF, Cliford Mario Ndimbo kwa niaba ya Kamati ya Maadili ambayo iko chini ya Mwenyekiti Hamad Mbwezeleni ametaja makosa hayo kuwa ni 

1. Kupokea/Kuchukuwa fedha za Shirikisho (TFF) za malipo ambayo hayakuwa halali ikiwa ni kinyume na kifungu cha 73(1) cha kanui za Maadili za TFF Toleo la 2013

 2. Kughushi barua ya kueleza alipwe malipo ya Kampuni ya JEKC SYSTEM LIMITED huku akijua malipo hayo sio halali ikiwa ni kinyume na kifungu cha 73(7) cha Kanuni za Maadili za TFF Toleo la 2013 

3. Kufanya Vitendo vinavyoshusha hadhi ya Shirikisho ikiwa ni kinyume na Ibara ya 50(1) ya Katiba ya TFF (Kama ilivyorekebishwa mwaka 2015). 

Kamati ya Maadili ya TFF iliyoketi jana Machi 14 imemfungia Michael Wambura maisha kutojihusisha na soka baada ya kujiridhisha kuwa ametenda makosa tajwa hapo juu ikumbukwe katika Soka la Tanzania Wambura Huyu Huyu aliwahi kufungiwa na klabu ya Simba kutokana na kupeleka maswala ya Soka mahakamani. 

No comments

Powered by Blogger.