JOHN BOCCO NDIE MCHEZAJI BORA MWEI JANUARI LIGI KUU


Nahodha wa timu ya Simba John Bocco amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kwa mwezi Januari baada ya kumpiku nyota mwenzake Emmanuel Okwi na Awesu Awesu wa Mwadui FC.
Bocco amecheza mechi tatu mwezi Januari akifunga mabao matatu na kusaidia mengine mawili huku akicheza dakika zote 270..
John  Bocco atazawadiwa tuzo, kisimbuzi cha Azam TV na fedha taslimu sh. milioni moja kutoka kwa mdhamini mkuu wa ligi kampuni ya Vodacom Tanzania.

No comments

Powered by Blogger.