COUTINHO AFUNGUA UKURASA WA MABAO, BARCELONA IKITINGA FAINALI COPA DEL REY

Lionel Messi was the first to congratulate the former Liverpool man on his first goal for the Catalan club 
Mshambuliaji wa barcelona Phillipe Countinho Jana usiku alifungua ukurasa wa mabao katika klabu yake hiyo mpya aliyojiunga nayo akitokea Liverpool baada ya kufunga moja ya mabao mawili ambayo Barcelona waliyapata jana katika ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Valencia katika kombe la Mfalme.

Countinho alianzia benchi katika mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Mestalla ukiwa ni mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya kombe la Mfalme maarufu kama Copa del Rey huku mchezo wa awali uliipa Barcelona faida baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Phillipe Countinho aliingia kipindi cha pili kilipoanza akichukua nafasi ya Andre Gomes na dakika tatu baadae akaweza kuifungia timu yake bao la kwanza baada ya kipindi cha kwanza kumalizika ikiwa ni bila bila. Bao la pili la barcelona lilifungwa na Ivan Rakitic dakika ya 82 kukamilisha ushindi huo ambao unaipa barcelona tiketi ya kucheza fainali ya kombe hilo dhidi ya Sevilla.

No comments

Powered by Blogger.