YANGA NA SIMBA KUANZA NA VIBONDE CAF

Droo ya kupanga ratiba ya michuano ya kimataifa ya vilabu barani Afrika imefanyika leo mchana kwa timu za Tanzania kupangiwa wapinzani wao katika michuano hiyo
Yanga ataanza kuchuana na St Louis ya Shelisheli, Yanga wakishinda mchezo huo  watakutana na Mshindi wa mchezo kati ya Township Rolers ya Botswana au Merrikh ya Sudan.

Simba wao wataanza na Gendarmerie ya Djibouti na wakifanikiwa kushinda mchezo huo watakutana na Green Buffaloes ya Zambia au El Masry ya Misri 

Wawakilishi kutoka Zanzibar timu ya JKU imepangiwa Zesco United ya Zambia ambayo nayo itaanzia nyumbani.
Zimamoto ambayo itashiriki michuano ya Shirikisho Afrika kutokea Zanzibar imepangiwa timu ya Wolaitta Dicha ya Ethiopia.

Mechi za awali zifanyika Februari 9-11 na marudio yatakuwa Februari 16-18.

No comments

Powered by Blogger.