MBARAKA KUELEKEA SAUZI KESHO KWA MATIBABU

MSHAMBULIAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Mbaraka Yusuph, anatarajia kuondoka nchini kesho Jumatano jioni kuelekea jijini Cape Town, Afrika Kusini kwa uchunguzi wa goti lake la kushoto baada ya kuumiza ‘meniscus’ (washa).

Yusuph alipata majeraha hayo akiwa na timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ wakati ikicheza na Libya kwenye mchezo wa michuano ya Kombe la Chalenji ulifanyika nchini Kenya Desemba 3 mwaka huu.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo, Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd, alisema kuwa tayari uongozi wa timu hiyo wameridhia na atakwenda sambamba na Makamu Mwenyekiti, Abdulkarim Nurdin ‘Popat’, atakayekuwa akishughulikia taratibu zake zote za matibabu.

“Mbaraka atakwenda kufanyiwa kwanza uchunguzi zaidi baada ya kupata uchunguzi wake na kupata majibu kwamba ni kitu gani kinamsumbua zaidi wao ndio watajua kuwa Mbaraka anahitaji operesheni au atapewa tiba mbadala,” alisema.

No comments

Powered by Blogger.