KENYA WATWAA UBINGWA WA CECAFA
Timu ya Taifa ya Soka ya Kenya wametawazwa mabingwa
wa michuano ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati 'CECAFA' kwa kuifunga
Zanzibar jumla ya penati 3-2 baada ya dakika 120 kumalizika kwa Sare ya 2-2.
Mpaka mapumziko Kenya walikuwa mbele kwa bao
moja kwa bila, Kipindi cha pili Zanzibar Heroes walikuja wakiwa na ari zaidi
wakitafuta bao la kusawazisha na pengine kupata bao la ushindi.
Khamis Mussa aliisawazishia Zanzibar dakika ya 87 baada ya
kumalizia mpira wa krosi na mlinzi wa kushoto Hajji Mwinyi.
Wenyeji walipata bao la pili dakika ya 97 kupitia kwa Choka Masoud kabla ya Khamis kusawazisha tena dakika mbili baadae.
Wachezaji wa Zanzibar Heroes waliokosa penati ni Adeyun Saleh, Issa Dau, Mohammed Issa 'Banka' wakati Feisal na Mudathir wakifunga.
Penati za Kenya zilifungwa na Atudo Otieno, Onguso Arasa na Ouma Onyango wakati Otieno Duncan akikosa penati yake.
Wenyeji walipata bao la pili dakika ya 97 kupitia kwa Choka Masoud kabla ya Khamis kusawazisha tena dakika mbili baadae.
Wachezaji wa Zanzibar Heroes waliokosa penati ni Adeyun Saleh, Issa Dau, Mohammed Issa 'Banka' wakati Feisal na Mudathir wakifunga.
Penati za Kenya zilifungwa na Atudo Otieno, Onguso Arasa na Ouma Onyango wakati Otieno Duncan akikosa penati yake.
No comments