TAIFA STARS KAMILI KUIVAA MALAWI LEO
Timu ya Soka ya
Tanzania maarufu kama Taifa Stars leo inacheza mchezo wa kirafiki dhidi Malawi jijini
Dar es salaam katika Uwanja wa Uhuru.
Kiingilio katika
mchezo huo wa kirafiki ni elfu 3,000 mzunguko na jukwaa kuu 5,000
Kocha wa Taifa Stars Salum
Mayanga amesema Vijana wake wapo tayari kutokana na maandalizi mazuri
waliyofanya kwa wiki nzima na kikosi chake.
Amewaomba watanzania
waje kwa wingi kuisapoti timu hiyo ambayo inajiandaa na mechi za kufuzu Afcon
2019.
No comments