NGOMA,TAMBWE,KAMUSOKO NDANI JUMAMOSI DHIDI YA MNYAMA

Benchi la ufundi la timu ya Yanga limepata uhueni baada ya wachezaji wake watatu Amiss Tambwe,Donald Ngoma na Thaban Kamusoko kujiunga na wenzao kambini baada ya kupona majeruhi

Kikosi cha Yanga kipo kambini mkoani Morogoro kwa ajili ya kujiandaa na mchezo dhidi ya watani wao wa jadi Simba utakaofanyika kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam Jumamosi ijayo.

Nyota hao raia wa kigeni walikuwa majeruhi kwa muda wakikosa baadhi ya mechi huku Tambwe akiwa hajapata nafasi ya kucheza mechi hata moja mpaka sasa.

Msemaji wa klabu hiyo Dismas Ten amesema wachezaji hao wamejiunga na wenzao kambini mkoani Morogoro leo tayari kwa mchezo huo.

"Wachezaji wetu Ngoma, Tambwe na Kamusoko wamejiunga kambini leo na wenzao mwalimu atakapoona inafaa kuwatumia kutokana na kupona majeraha," alisema Ten.


Timu zote zina pointi 15 huku Simba ikiongoza kwa idadi ya mabao ya kufunga.

No comments

Powered by Blogger.