NCHI TATU ZAGOMBEA UENYEJI CHAN

Shirikisho la soka barani Afrika (Caf) limethibitisha kupokea maombi ya nchi tatu ambazo ni Equitorial Guinea, Ethiopia na Morocco wametuma maombi ya kuandaa mechi za taifa bingwa barani Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN).
Morocco ilithibitisha ombi lao siku ya Jumamosi, nao Caf wakatangaza jana Jumapili kuwa pia kulikuwa na maombi kutoka nchini Ethiopia na pia Equitorial Guinea, ambao waliandaa mechi za taifa bingwa barani Afrika mwaka 2015.

Caf wanatafuta mwenyeji mpya kuchukua nafasi ya Kenya ambayo ilipoteza fursa hiyo baada ya kushindwa kutimiza matakwa ya shirikisho la Caf

No comments

Powered by Blogger.