USHANGILIAJI ULIOACHA HISIA TOFAUTI KWA MASHABIKI
Kila mchezaji anapoingia uwanjani kucheza matarajio yake ni
ushindi, lakini ushindi dhidi ya timu yako ya zamani huwa na hisia za kipekee
kabisa. Kuifunga timu yako ya zamani siyo jambo la kushangaza kabisa lakini
namna unavyoshangilia baada ya kuifunga tiu yako ya zamani ndiyo huwa kinaibua
maswali mengi na hisia tofauti kwa wapenzi wa mpira wa miguu.
Wapo waliozifunga timu zao za zamani lakini waliishia
kunyanyua mikono juu ishara ya kuomba msamaha, lakin wapo wengine waliofunga
timu zao za zamani wakaishia kushangilia kana kwamba hawajawahi kuchezea timu
hizo. Kushangilia huko mara nyingine kunakuwa ni kama kupigilia msumari wa moto
kwenye vifua vya mashabiki wa timu iliyofungwa. Lakini pia wapo wachezaji
wachache ambao mashabiki wanafurahia hata wakifungwa na wachezaji hao.
Tumekuwekea hapa wachezaji wachache waliowahi kushangilia
baada ya kuzifunga timu zao za zamani. Wachezaji hao walishangilia kwa hisia na
kupeleka ujumbe kwa mashabiki wakati mwingin kupelekea mashabiki kuwachukia
wachezaji hao.
1.
Robin van Persie: Manchester United vs Arsenal
Baada ya kufunga magoli 132 katika misimu 8 aliyodumu
Arsenal, Robin van Persie aliamua kutafuta maisha mapya ambayo yatampa furaha
zaidi. Kocha wa Manchester United wakati huo Sir Alex Ferguson aliamua
kumkaribisha Robin van Persie katika viunga vya Old Trafford kuja kujaribu
bahati yake.
Robin alijaribu kuzuia hisia zake alipoifunga Arsenal katika
dimba la Emirates, Lakini katika dimba la Old Trafford Robin alionyesha furaha
ya aina yake mara baada ya kuifunga Arsenal akiunganisha kwa kichwa mpira
uliopigwa na Wayne Rooney. Robin baada ya kufunga goli hilo alinyanyua mikono
juu na kushangilia huku akimkimbilia Wayne Rooney ili wafurahie pamoja. Ilikuwa
ni furaha ya aina yake lakini mwiba mkali sana kwa mashabiki wa Arsenal hasa
baada ya kushuhudia mafanikio aliyoyapata Van Persie mara baada ya kuondoka
Arsenal.
2.
Danny Welbeck: Arsenal vs Manchester United.
Amekuzwa na kufundishwa soka chini ya Manchester United,
Usajili wake haukuwavutia mashabiki wengi wa Arsenal. Msimu wake wa kwanza kwa
Arsenal haukuwa mzuri kutokana na kutawaliwa na majeruhi sana. Lakini aligeuka
lulu hasa pale alipofunga goli muhimu lililopeleka Arsenal Nusu fainali na
walifanikiwa kufika fainali na kuchukua kikombe cha Ligi (FA CUP) Msimu huo.
Welbeck atakumbukwa sana mara baada ya kuifunga timu yake
iliyomlea na kumkuza Manchester United. Lakini nay eye welbeck hakuishia
kufunga tu, bali alishangilia kuashiria kuwa yuko na furaha katika klabu ya
mpya. Lilikuwa ni goli moja tu ambalo liliiondoa Manchester United katika
mashindano hayo na furaha ya Welbeck ilikuwa juu zaidi hasa baada ya kuifunga
Manchester United katika uwanja wao wa nyumbani Old Trafford.
3.
David Luis: PSG vs Chelsea
Hakujali misimu kadhaa aliyokaa Darajani kwa Chelsea,
Hakujali Sura zilzile alizokuwa nazo bega kwa bega kupambana na miamba mingine
ya ligi kuu England, kilichokuwa muhimu kwake ni Ushindi Klabu yake ya PSG.
Huyo ndiye David Luis, Goli lake halitakuja kusahaulika kwani ni moja ya magoli
yaliyozamisha meli yay a Chelsea na kushindwa kuvuka hatua ya 16 bora ya ligi
ya klabu bingwa Ulaya.
Lakini hasira za mashabiki ziliisha na waliweza tena
kumpokea kijana wa alipoamua kurudi nyumbani darajani mwaka 2016 akitokea
katika klabu ya PSG kwa dau la £34m.
4.
Emmanuel Adebayor: Manchester City vs Arsenal
Katika msimu wa 2007/2008 Adebayor alifanikiwa kuifungia
Arsenal magoli 30 katika mashindano yote, alikuwa mwiba kweli kwa timu pinzani.
Lakini upendo wake ulitiliwa shaka alipokubali kuondoka London na kwenda
kujiunga na Manchester City kwa dau la £25m.
Mashabiki wa Arsenal hawakufurahishwa na kitendo cha
Adebayor kuhama kuondoka Arsenal, lakini Adebayor aliwakera zaidi baada ya
kupiga usoni kipenzi chao Van Persie na alipelekea kufungia mechi tatu. Chakukumbwa
zaidi katika mechi hiyo ni tukio alilolifanya Adebayor mara baada ya kuifunga
Arsenal katika mechi hiyo.
Ulikuwa ni ushangiliaji wa aina yake na wenye hisia kali.
Adebayor hakujali kuwa hawa walikuwa ndugu zake miezi kadhaa nyuma, hakujali
namna walivyomshangilia wakati yupo nao, yeye alichojali muda ule ni kuonyesha
hisia zake juu ya goli alilofunga. Mara baada ya goli hilo Adebayor alikimbia
na kushangilia mbele ya mashabiki wa Arsenal na Alipoulizwa kwanini aliamua
kushangilia vile, Adebayor alijibu ile ilikuwa ni kulipa kisasi kwa namna
mashabiki wa Arsenal walivyokuwa wanadhihaki kwa kitendo chake cha kuhamia
Manchester City.
Ni hayo tu kwa leo, je ni mchezaji gani unayemkumbuka ambaye naye aliwahi kushangilia mara baada ya kuifunga timu yake ya zamani.
Tuandikie maoni yako hapo chini kwenye kisanduku cha maoni.






No comments