UCL : ARSENAL UGENINI KUVAANA NA PSG,MAN CITY NA WAJERUMANI

Msimu mpya wa ligi ya mabingwa Barani Ulaya hatua ya makundi inaanza leo usiku kwa michezo nane kupigwa katika viwanja tofauti.


Arsene Wenger akiwa na Arsenal yake atakua jijini Paris kumenyana na matajiri wa jiji la Paris klabu ya PSG mchezo wa kundi A katika dimba la Parc de Prince mchezo unaotajwa kuwa mgumu kwa timu zote kutokana na uimara wa vikosi vyao.

Pep Guadiola akiwa na furaha ya ushindi dhidi ya Manchester United usiku wa leo atakua nyumbani katika dimba la Etihad zamani City of Manchester kucheza na Borussia Mongledbach ya Ujerumani.

Celtic inayofundishwa na Brendan Rodgers itakua ugenini kucheza na Mabingwa wa SPAIN Barcelona ambao weekend iliyopita walipigwa bao 2-1 katika ligi kuu huku Celtic ikishinda bao 5-1 katika ligi ya Scotland.

RATIBA KAMILI YA MECHI ZA LEO

KUNDI A

Basel v Ludo Razgrad            
Paris St Germaine v Arsenal                

KUNDI B

Benfica v Besiktas          
Dynamo Kiev v Napoli              

KUNDI C

Barcelona v Celtic          
Man City v Borussia Monchengladbach          

KUNDI D

Bayern Munich v FC Rostov                
PSV Eindhoven v Atletico Madrid

NOTE: MECHI ZOTE HIZI ZITAANZA SAA 3 NA DAKIKA 45 USIKU

No comments

Powered by Blogger.