BARCELONA YAMTAMBULISHA MRITHI WA KIPA CLAUDIO BRAVO

Mabingwa wa Spain Barcelona wamemtambulisha kipa wao mpya Jasper Cillessen waliyemsajili toka Ajax Amsterdam.


Jasper mwenye miaka 27 amesaini miaka minne kuichezea Barcelona kwa uhamisho wa Euro milioni 13

Anakua mchezaji wa 5 kusajiliwa na Barcelona kipindi hiki cha usajili baada ya usajili wa Denis Suarez, Lucas Digne, Samuel Umtiti na Andre Gomes na anaweza kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Atletico Bilbao Jumapili baada ya Andre ter Stegen kuwa majeruhi.

Golikipa huyo amejiunga na Barcelona akiziba nafasi ya Claudio Bravo aliyetimkia Manchester City.

No comments

Powered by Blogger.