LICHA YA KUINGIZA BURE MASHABIKI,YANGA YAKUMBANA NA KICHAPO TAIFA

 Mechi ya pili ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika baina ya Mabingwa wa Tanzania Bara Yanga na mabingwa wa Afrika TP Mazembe limemalizika kwa Yanga kuambulia kichapo cha bao 1-0.


Pambano hilo lilichezwa katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam halikua na kiingilio kwa mashabiki waliojitokeza kulitazama  na hivyo kupelekea uwanja huo wenye uwezo wa kujaza mashabiki 60,000 kujaa

Mpaka mapumziko Hakuna timu iliyofanikiwa kuliona lango la timu pinzani na kupelekea matokeo kubaki bila bila.

Kipindi cha pili Tp Mazembe walionekana kuwa bora zaidi na kuwazidi ujanja Yanga wakipata bao pekee dakika ya 74 likifungwa na  mlinzi wa Mazembe raia wa Congo Merveille Bope Bokad74

Kwa matokeo hayo Tp Mazemne wanaongoza kundi A wakiwa na pointi 6 na Yanga ni ya mwisho.


No comments

Powered by Blogger.