KOMBE LA CHALENJI : RWANDA YAFUZU ROBO FAINALI ZANZIBAR HEROES YAKUMBUKA SHUKA ASUBUHI

Michuano ya kombe la  CHALENJI 2015 imeendelea leo ijumaa kwa michezo kadhaa kupigwa katika kukamilisha hatua ya hatua ya makundi.


 Michuano inayopigwa nchini Ethiopia ilishuhudiwa leo  Rwanda wakiwashushia kapu la magoli vibonde  somalia, na kufuzu hatua ya robo fainali kwa kuitandika bao 3-0 katika mchezo huo uliokuwa wa upande mmoja zaidi.

Katika mchezo mwingine wawakilishi wa Tanzania visiwani Zanzibar Heroes walistuka kutoka usingizini na kuwashushia timu ya taifa ya Kenya Harambee stars kwa kuwafunga bao 3-1 matokeo ambayo ni faraja tu kwa Zanzibar kwani ilishatupwa baada ya kupoteza michezo yake ya awali.

MATOKEO YOTE YA MECH ZA LEO
Rwanda 3 – 0 Somalia
Zanzibar 3 – 1 Kenya
South Sudan 2 – 0 Mal;awi

No comments

Powered by Blogger.