MTOTO WA DAVID BECKHAM KUKIPIGA ARSENAL 

Brooklyn na Tiago Silva
Si mara zote kile anachokipenda baba basi na mtoto akipende ndivyo ilivyo kwa Brooklyn David Beckham mtoto wa kwanza wa gwiji wa zamani wa klabu ya Manchester United David Beckham ambaye mapenzi yake kwa klabu ya Arsenal yakichangiwa pia na uwezo binafsi awapo uwanjani umewavutia jopo la wasaka vipaji wa klabu hiyo ya London kutaka kumsajili mazima mchezaji huyo ambaye amefanya vizuri katika mazoezi ya Arsenal na hasa akicheza katika timu ya vijana ya Arsenal chini ya miaka 16.


Brooklyn mwenye miaka 15 amewafurahisha makocha wa Arsenal na kuna mpango wa kumpa mkataba wa muda mrefu wakati atakapofikia miaka 16 mwezi March mwaka 2015 wakati ambao Arsenal wanaweza kumsajili kama mchezaji wa Academy na akifikisha miaka 17 anaweza kusaini kama mchezaji wa kulipwa kutokana na sheria ya soka.

Brooklyn amekua akiwaniwa kwa karibu mno na Klabu za Manchester United na Chelsea lakini ameonekana moyo wake una mapenzi na Arsenal na ameshawahi kufanya mazoezi na Manchester United, Chelsea na Fulham

Sio tu Brooklyn bali hata mdogo wake Romeo David Beckham mwenye miaka 12 ameonekana lulu katika mazoezi ya kikosi cha Arsenal chini ya miaka 13.
Brooklyn,David,Cruz na Romeo(Becks family)

Beckham na familia yake wanaishi London ambako nyota huyo aliyewika akiwa na Man United,Real Madrid na LA Galaxy ana bonge la mjengo.

+++++++++++++++++++++++++++++++

No comments

Powered by Blogger.