VAN GAAL HUWEZI KUPIKA CHAPATI KWA UNGA WA MUHOGO
Tunamshukuru aliyeleta wazo la kila kata kuwa
na shule ya sekondari. Shule hizi kwa
kiasi zimesaidia kufuta ujinga kwa walio wengi.Asilimia kubwa ya wanaomaliza shule
za msingi wanapata nafasi za kuingia kidato cha kwanza tofauti na enzi zile za
mwalimu na mzee Ruksa.
Heri nusu shari kuliko shari kamili,Ingawa shule hizi zina walakini lakini mchango wake kwenye jamii unaonekana. Tofauti ya sasa na zamani inaonekana kupitia shule hizi. Wengi hawajaelimika ila wamepunguza shari kwa kufuta ujinga. Wengi wao angalau wanajua kujieleza kwa lugha ya chakula,Pia wengi wanajua ukichanganya hydrogen na oxygen unapata maji,ukichukua sodium na chlorine unapata chumvi na ukitaka kupata chumvi na maji kwa pamoja ni lazima uchanganye acid na base.
Heri nusu shari kuliko shari kamili,Ingawa shule hizi zina walakini lakini mchango wake kwenye jamii unaonekana. Tofauti ya sasa na zamani inaonekana kupitia shule hizi. Wengi hawajaelimika ila wamepunguza shari kwa kufuta ujinga. Wengi wao angalau wanajua kujieleza kwa lugha ya chakula,Pia wengi wanajua ukichanganya hydrogen na oxygen unapata maji,ukichukua sodium na chlorine unapata chumvi na ukitaka kupata chumvi na maji kwa pamoja ni lazima uchanganye acid na base.
Hi ndio tunaita chemistry(kemia), kwa ufupi
kemia ni masomo ya atomi na mkusanyo wa atomi kuwa molyekuli. Yaani hizo atomi
ukizichanganya utapata kitu kizima kinachoitwa molyekuli, Hata ndugu zangu wajenzi wanajua ili upate zege lazima
uchanganye ingredients(vitu vinavyounda zege),Ili upate zege lazima uchanganye
maji, kokoto,mchanga na simenti kwa viwango maalumu.
Kwenye soka tumekuwa tukitumia maneno kama chemistry(kemia)
huku wengi tukiwa hatujui chimbuko lake. Mchezaji ndiyo atomi yenyewe na timu
ndio molyekuli. Kitendo cha kuwaunganisha wachezaji katika timu moja na
wachezaji hao kuungana katika mfumo husika ndio tunaita chemistry(kemia). Kocha
anaposhindwa kupata wachezaji husika kwenye mfumo husika hapo ndipo tunasema
kashindwa kutengeneza chemistry kwenye timu.
Kocha wa Manchester United Louis van Gaal kama hakukimbia somo la chemistry basi anataka kutuonyesha staili mpya ya kupika chapati kwa unga wa muhogo.Van gaal amethubutu kutengeneza molyekuli ya 3-5-2 lakini amekosa atomi husika za kutengeneza chemistry. Watu wa mpira wanaelewa kuwa nafasi ya kiungo ndio muhimu kuliko nafasi nyingine uwanjani. Kama unavyojua tafsiri ya Kiswahili ya neno kiungo pia ndio hivyo hivyo tafsiri hiyo hutumika katika soka.
Louis van Gaal anajaribu kutuelewesha Darren fletcher ni mtu sahihi kwenye safu yake ya kiungo lakini Garry Monk (kocha wa Swansea) na Gus Poyet (Kocha wa Sunderland) wametuonesha uongo wa Louis van Gaal.
Na kama kocha huyo ataendelea kuwa king’ang’anizi na stori yake ya fletcher na Tom Cleverely basi ategemee watu kuendelea kupiga miayo na wakiichoka stori yake watamkimbiza kama hakukimbia mwenyewe.
Manchester United imemsajili
Angel di Maria ambaye ni mchezaji bora wa Real Madrid nyuma ya Ronaldo na Bale
lakini kiungo huyo si dawa ya gonjwa la united. Hapa van Gaal anajaribu kusoma
vizuri stori ya dokta wa muhimbili aliyemfanyia mgonjwa upasuaji
wa kichwa baada ya mguu. Kama ni ukimwi di Maria ni ARV. Ataongeza kitu
katika timu ila hatatibu gonjwa la united. Manchester united inahitaji kiungo
mkabaji mwenye roho ngumu mithili ya Nigel de Jong.Kiungo mwenye kariba ya de
jong akisimama vizuri na Ander Herrera hapo ndipo utaona makali ya Wayne Rooney
na Robin van Persie. Kwa sasa washambuliaji hao
wanaonekana si lolote si chochote kwasababu ya atomi walizounganishwa nazo.
Ukiacha kupwaya kwenye nafasi ya
kiungo Manchester united imepwaya pia kwenye nafasi ya mabeki baada ya
kuondokewa na wakongwe Nemanja vidic,Patrice Evra na Rio Ferdinand. Tegemeo pekee
kwenye nafasi ya mabeki wa kati ni John Evans na Phil Jones. Hapa napo van Gaal
inabidi apatazame kwa mapana na marefu kama anataka kuirudisha united ya sir Alex Ferguson.
Manchester haina tatizo la
washambuliaji wala viungo wasaidizi wa washambuliaji bali wana tatizo la Kiungo
mkabaji na mchezeshaji sambamba na mabeki wa kati.Haihitaji vyeti kugundua
matatizo hayo.Macho yangu hayahitaji kuvaa miwani na hasilani hayanidanganyi.
Nakubali sina elimu ya ukocha kama Van Gaal ila hata yeye mwenyewe alikili kuwa timu yake haina uwiano
mzuri(imekosa balance),wala siwezi ishi ndani ya kichwa cha Van Gaal kujua nini
kapanga juu ya hatima ya Manchester united
ila ninachoweza kumwambia au kumkumbusha Van Gaal ni kuwa kamwe hawezi
kupika chapatti kwa unga wa muhogo..
Alleen kaijage
0655106767
kaijagejr@gmail.com
No comments