WACHEZAJI WA 5 WATANGAZWA
Yaya Toure, kwa mwaka wa pili mfululizo, yupo kwenye orodha hiyo.
Mwenzake katika timu ya taifa ya Ivory Coast, Didier Drogba pia yumo.
Wachezaji wengine ni pamoja na Demba Ba kutoka Senegal, Younes Belhanda wa Morocco na nahodha wa timu ya Zambia, Christopher Katongo.
Huu umekuwa ni mwaka wa ufanisi kwa wachezaji hao, na timu za wachezaji wanne zikionyesha ustadi kwa kupata vikombe.
Inaelekea Drogba aliondoka Chelsea wakati muwafaka, mara tu baada ya timu yake kukamilisha msimu kwa ushindi wa klabu bingwa barani Ulaya, hii ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya klabu, na vile vile akipata bao la ushindi katika fainali ya Kombe la FA.
Wanaowania tuzo la BBC
Yahya Toure.Mcheza kiungo kutoka Ivory Coast,
anayeichezea Manchester City ya Uingereza. Toure aliiongoza Manchestert City
kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya
miaka 44 iliyopita.
Demba Ba kwa sasa ni mmoja wa wachezaji nyota
wa klabu ya Newcastle na kufikia sasa tayari amefunga jumla ya magoli 6 katika
ligi kuu ya premier la England na anatarajiwa kujumuishwa kwenye kikosi cha
Senegal kitakachocheza katika fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika.
Didier Drogba ni noadha wa timu ya taifa ya
Ivory Coast, amewahi kuongoza Chelsea kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya
England pamoja na kombe la klabu bingwa barani ulaya.
Christopher Katongo ni mchezaji wa timu ya
taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo na aliiongoza timu hiyo kushinda
fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika
Bofya Younes Belhanda ni
mchezaji mwenye umri wa miaka 22, na mmoja wa wachezaji waliotia fora na
kuisaidia klabu ya Montepellier, kushinda kombe la ligi kuu kwa mara ya kwanza
kwa zaidi ya karne moja tangu klabu hiyo ilipobuniwa.
Kwa Habari kamili Tembelea bbc swahili
No comments