UPAMBE
WA KAIJAGE KWENYE HARUSI YA KISPANYOLA,ZURICH(part 1) ...... Nashukuru
mungu kwa kunipa nafasi ya kua mmoja wa wapambe kwenye harusi hii ya
kispanyola huko zurich,kwenye harusi kuna watu wengi mashuhuri lakini
bibi na bwana harusi ndo mabosi wa sherehe.. Hata ukiwa maarufu kiasi
gani.. Jina la bibi na bwana harusi vitatawala mdomoni mwa mc..... Bibi
na bwana harusi watakua bora kuliko watu wote harusini....Nimehudhuria
harusi nyingi lakini hii naisubiri kwa hamu...harusi hii ni ya ajabu
..harusi hii inanikumbusha kitabu kimoja pendwa kiitwacho "three suitors
one husband" ... Kwenye hii harusi kuna madume watatu lakini anatakiwa
mume mmoja tu.... Cha ajabu midume yote inajiona inastahili kumchukua
mwanamwali.....pia mwanamwali anaona anastahili kuolewa na mwanaume
yeyote kati ya hao watatu ...hama kweli hii ni harusi ya dunia....
Madume hayo yametoka sehemu tofauti japo yote yamelowea spain.. Dume la
kwanza kutoka Argentina mloezi wa spai
n,la
pili kutoka portugal pia mloezi wa spain na Dume la mwisho ni kutoka
spain... Kila Bwana harusi amekuja na wapambe wake.... Na kila mpambe
anataka dume lake ndo lichukue mwanamwali..... Ikambidi mzazi wa bibi
harusi Aitwaye seif blatter mkazi wa zurich atumie busara na
hekima.....Dunia nzima ikawa na shahuku ya kusikiliza nini mzazi wa bibi
harusi atasema kuhusiana na ndoa ya binti yake.. Mzazi huyo wa bibi
harusi akaamua kuunda kundi dogo la watu ambao wanajua sifa za bwana
harusi bora... Wachunguze kisha wapige kura yupi anafaa kuondoka na
mwanamwali..... Uamuz huo wa busara kabisa kuchukuliwa na wazazi wa
upande wa bibi harusi kwa pamoja (fifa)..... Kundi hilo au kamati hiyo
itaangalia nini kila bwana harusi alifanya kwa mwaka mmoja ulopita ili
astahili kuitwa mwanaueme bora kuliko wenzake..... Kuna njia nyingi za
kujua wewe ni mwanume au mume bora....Lakini cha kustahabisha Wanaume
hawa wamefanana kwa vitu vingi sana maumbo,sura pia hata mvuto Lakini
pia Bahati ilioje wote wamejikuta ni wasakata kabumbu.... Hyo ndo ikawa
sifa kubwa na ya pekee kujua na kuwatofatisha yupi ni bora kati yao...
Basi Kamati ikaamua Iegemee katika sifa ya kusakata mpira wa miguu....
Nilivyosikia hvyo nikastaajabu nikisema moyoni ni hekima ya namna gani
mungu amewajaria wazazi wa bibi harusi. inafanana na hile ya
meshack,shadrak na abednego na pia kidogo kutoka kwa suleiman..... Sasa
ikafika zamu ya kamati kuletewa sifa za kila mmoja kuzichambua kabla ya
kupiga kura...................... To be continue(itaendelea)...................................................................

Sawa mpambe, tupe umbea
ReplyDeleteSawa
ReplyDelete