HUYU NDIYE KOCHA MPYA WA SIMBA


Simba SC imeingia mkataba na kocha Dylar Kerr Raua wa England kuifundisha klabu hiyo kongwe nchini ambayo ilimaliza Ligi ikiwa katika nafasi ya tatu.

Kerr atasaini mkataba wa mwaka mmoja kuinoa Simba mkataba ambao una kipengele cha kuongeza mwaka mwingine kama atafanya vizuri.

Kocha huyo anakuja Simba SC akitokea klabu ya Ligi Kuu ya Vietnam, Hai Phong aliyojiunga nayo Januari mwaka 2014.

Amezaliwa January 14 mwaka 1967 katika kitongoji cha Valletta nchini England

Kerr amewahi kucheza katika ligi kuu ya England hususani vilabu vya Sheffield Wednesday na Leeds United akicheza kama beki wa kushoto.

No comments

Powered by Blogger.