UVUMILIVU UMEWASHINDA, EVERTON WAMTUPIA VIRAGO KOEMAN

Klabu ya Everton imeshindwa kumvumilia kocha wao Ronald Koeman baada ya kumtimua kufuatia vigigo vya mfululizo wanavyoendelea kuvipata.

Everton imeshinda mechi mbili pekee za ligi msimu huu ikiwa nafasi ya 18 kwenye msimamo na pia wakiburuza mkia kwenye kundi E katika michuano ya Europa.


Kipigo cha mabao 5-2 walichokipata jana kutoka kwa Arsenal na kile cha mabao 2-1 dhidi ya Olympic Lyon kwenye michuano ya Europa vimechangia kwa kocha huyo raia wa Uholanzi kutupiwa virago hii.

Klabu hiyo imetangaza maamuzi hayo mchana wa leo baada ya Mwenyekiti wake Bill Kenwright na Mkurugenzi mtendaji Robert Elstone kuwasili kwenye uwanja wa mazoezi wa mazoezi wa timu hiyo.


Kocha wa timu ya vijana ya miaka 23 David Unsworth atakaimu nafasi hiyo kwa muda ambapo watasafiri kucheza na Chelsea katika kombe la ligi keshokutwa Jumatano kabla ya kukutan na Leicester City Jumapili ijayo.

No comments

Powered by Blogger.